Friday, September 17, 2010

JE QURANI INAAMURU WATU KUVUA VIATU WAKATI WA IBADA?


JE QURANI INAAMURU WATU KUVUA VIATU WAKATI WA IBADA?




Mwadishi: Ustadh Chaka Ibn Moosa:
Mhariri: Joseph Kimonyi
Barua pepe:abdulhaq2099@yahoo.com

Utangulizi
Mara nyingi sisi wakristo tumeshutumiwa sana na waislamu kwa kutotoa viatu wakati wa ibada. Kuna vikundi vingi sana vya waislamu hasa waendeshaji mihadhara, vikundi hivi vinazunguka sehemu mbalimbali wakifundisha watu kuwa nilazima watu kutoa viatu wakati wa ibada, Kwani hata Manabii wa zamani walifanya hivyo. Na ukiwauliza ni wapi qurani inaamuru kutoa viatu wanakuwa wakali. Swali la kujiuluza, je ni kweli au ni uongo. Fuatilia somo hili ili upate kufahamu.

Al'Hajj 22:67 (kuhiji)
“Kila umma tumeujalia kawaida ya ibada wanayoishika. Basi wasishindane nawe katika jambo hili. Na walinganie watu kwendea (Dini ya) Mola wako. Bila shaka wewe uko juu ya uongozi uliosawa kabisa.”

Kama waislamu wangalijua maana ya aya hii, wasingalipiga makelele. Kwani Mungu wao Allah anasema kuwa kila umma ameujalia kawaida ya lbada. Kwani kila umma una ibada tofauti umma mwingine.

Sehemu kuu ya somo hili
1. hoja za waislamu kuhusu kutoa viatu.
2. Kwa nini musa na Yoshwa akatoa viatu.
3. Je wakristo tuamurishwa kutoa viatu?
4. Je kuvua viatu ni ibada?

1. Hoja za waislamu kuhusu kutoa viatu.
Waislamu hupenda kutumia hoja zifuatazo kwa kudai kuwa zinamurisha watu kuvua viatu wakati wa ibada.

Kutoka 3:4-6
“Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema Musa! Musa! Akasema mimi hapa. Naye akasema, usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali usimamapo ni nchi takatifu. Tena akasema mimi ni Mungu wa baba yako Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake maana aliogopa kumwangalia Mungu.”

Andiko lingine wanalolipotosha ni hili.
Yoshwa 5:13-14
“Ikawa hapo Yoshwa alipokuwa karibu na mji wa Yeriko, akavua macho na kuangalia, na tazama mtu mume akasimama akamkabili mbele yake, naye alikuwa na upanga wazi mkononi mwake; Yoshwa akamwendea, na kumwambia, je! wewe uko upande wetu au upande wa adui zetu? Akasema, la lakini nimekuja sasa, nili amiri wa jeshi la Bwana. Yoshwa akapomoka kiusouso hata nchi akasujudu, akamwuliza, Bwana wangu aniambia nini mimi mtumishi wake? Huyo amiri wa jeshi la Bwana akamwambia Yoshwa, vua viatu vyako miguuni mwako, kwa kuwa mahali hapo usimamapo ni patakatifu. Yoshwa akafanya vivyo.”
Hapa tunaona Musa na Yoshwa waliambiwa watoe viatu vyao, swali kwako wewe mwislamu unaotoa viatu wakati wa ibada. Je ni aya gani katika Qurani au Biblia inayokupa wewe ruhusa ya kutoa viatu, na kama hakuna amri hiyo mnatowa wapi.?
Wewe kama mwislamu tafakari aya zifwatazo kwa makini ili upate kuelewa.

Zaburi 139:7-12
“Niende wapi nijiepushe na roho yako? Niende wapi niukimbie uso wako? Kama ningepanda mbinguni, wewe uko; ningefanya kuzimu kitanda changu, wewe uko. Ningezitwaa mbawa za asubuhi, Na kukaa pande za mwisho za bahari; huko nako mkono wako utaniongoza, Na mkono wako wa kuume utanishika. Kama nikisema, hakika giza litanifunika, Na nuru inizungukayo imekuwa usiku; giza nalo halikuchi kitu, Bali usiku huangaza kama mchana; Giza na mwanga kwako ni sawaswa.” (Pia tazama lsaya 6:3; Yeremia 23:23-24; Mithali 15:11)

Kwa mjibu wa Biblia tunaona kuwa Mungu yuko kila mahali, kwani hatuwezi kujificha uso wa Mungu.Hebu tuangalie jinsi Qurani inavyofundisha.

Al-an'am 6:3
“Na yeye ndiye Mwenyezi Mungu katika mbingu na katika ardhi, na anaijua ndani yenu na nje yenu; anayajua (yote) mnayoyachuma.”

Al Baqarah 2:115
“Na mashariki na magharibi ni ya Mwenyezi Mungu. Basi popote mgeuliapo (alikokuamrisheni Mwenyezi Mungu mtazikuta) huko radhi za Mwenyezi Mungu. Bila shaka mwenyezi Mungu ni Mwenye wasaa (mkubwa kabisa) na mwenye kujua kukubwa (kabisa vile vile) (24:35)”

Kwa kuwa Mungu yuko kila mahali, naomba majibu kwa maswali fwatayo.
· Je Musa na Yoshwa waliweka wapi viatu vyao?
· Na kama Musa na Yoshwa walivishika mkononi, hakuwa najisi?
· Je pahali pale palikuwa mahali pa ibada kama msikitini?
Kando na hawa kunaye mwingine aliyeamurishwa kuvua viatu?
Kwa hivyo mwislamu kabla ya kuanza kuzungumza, ni lazima ujihoji kwa maswali hayo hapo juu, na utaona ya kuwa Mungu hakuwa na maana kama waislamu wanayoichukulia, kwani Mungu mwenyewe asema hivi.

Isaya 55:8
“Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema BWANA.”

2.kwa nini Musa naYoshwa wakatoa viatu.
Biblia inatufundisha ya kuwa wamesimama katika ichi takatifu. Mungu alikuwa na maana ya kujitakasa nafsi zao. Kwa mfano,

Walawi 11:44
“Kwa kuwa mimi ni BWANA, Mungu wenu; takaseni nafsi zenu basi; iweni watakatifu, kwa kuwa mimi ni mtakatifu; wala msitie uchafu nafsi zenu kwa kitu kitambaacho cha aina yoyote, kiendacho juu ya nchi. Kwa kuwa mimi ni BWANA niliyewaleta kutoka katika nchi ya misri, ili kwamba niwe Mungu kwenu; mtakuwa watakatifu, kwa kuwa mimi ni mtakatifu.

Mungu wetu mara nyingi hunena maneno ambayo katika hali ya mafumbo, na mtu wa mwili hawezi kufahamu. Kama vile, Mungu ametuambia kuwa tuzitahiri nyama ya govi ya roho zetu wala tusiwe wenye shingo ngumu. Kumbukumbu la Torati 10:16; Walawi 26:4; Yeremia 4:4; Wakolosai 2:11.mfano mingine wa kuangalia ni Ufunuo 2:7. Na mwenye sikio na asikie….

3. Je wakristo wameamriswa kutoa viatu?
Swala la msingi la kuchunguza ni jinsi Biblia inavyofundisha kuhusu viatu.
Kutoka 12:11
“Tena mtamla hivi, mtakuwa mefunga viuno vyenu, mmevaa viatu miguuni na fimbo zenu mikononi mwenu; nanyi mtamla kwa haraka ni pasaka ya Bwana.”

Kulingana na mafundisho ya Biblia hii ni ibada maluumu, na Mungu amesema kuwa watutakuwa wamevaa viatu. Fuatilia somo hili ili upate kujua ukweli wa mambo.

Kumbukumbu la torati 29:5
“Nami miaka arobaini nimewaongoza jangwani; nguo zenu hazikuchakaa juu yenu, wala kiatu chako hakikuchakaa katika mguu wako.”

Mungu kwa miaka arobaini alikuwa akiwaongoza katika jangwa huku wamevaa viatu mguuni mwao. Kwa hivyo tunaona jinsi Mungu alivyo mwingi wa rehema, kwani katika mila na desturi za kiyahudi ni lazima kila mtu avae viatu. Na ndiposa nabii Yeremia ansema hivi.
Yeremia 2:25
“Zuia mguu wako usikose kiatu, na koo yako isiwe na kiu…
Hata Yohana kwa ushuhuda wake anasema maneno haya.
Mathayo 3:11
“Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuniliko mimi, wala sisitahili hata kuvichukwa viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na moto.”

Kwa wakristo Bwana Yesu ndiye mfano mwema, kwani yeye ndiye njia na kweli na uzima mtu hawezi kumfikia Mungu bila Bwana wetu Yesu kristo. Yohana 14:6.

Je kunayo aya yoyote inayowaruhusu waislamu watoe viatu wakati wa ibada?.
Al-Ahzab 33:21
“Bila shaka mnao mfano mwema (ruwaza nzuri) kwa mtume wa Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho, na kutaja Mwenyezi Mungu sana.”

Kwa waislamu mfano wao mzuri ni mtume Muhammad, kwani alichokitenda inawapasa wao kukitenda. Hebu tuangalie jinsi mtume alivyokuwa akiswali, tukichunguza na vitabu vingine. Kwa sababu Qurani inaruhusu kusoma hata hadithi za mtume.
Ash-shura 42:10
“Mkihitilafiana katika jambo lolote (rejeleeni kitabu cha Mwenyezi Mungu na hadithi za mtume kwani) hukumu yake iko kwa Mwenyezi Mungu. Huyo Mwenyezi Mungu ndiye Mola wangu ninaye mtegemea, na kwake ninarejea.”

Hivyo kila mwislamu hata afanyenini ni lazima matamanio yake kama alivyotenda mtume. Na mojawapo ya yale alioyatenda ni kuswali huku amevaa viatu.

MISHKAT AL MASABIH VOL 1 SURA (CHAPTER) 10 SEHEMU 3.
Mtume alikuwa akisali huku amevaa viatu, Al Mughira alijaribu kumkumbusha Muhammad hasa pale alipomwona anatawadha juu ya viatu na kuingia navyo msikitini, hivyo Mughira akasema “Ewe Mtume wa Allah umesahau’’ Mtume akajibu kumwambia Al Mughira akisema “wewe ndiwe uliye sahau kwa maana hivi ndivyo alivyo niamuru Mungu.

Kama mtume aliambiwa aswali na viatu, mbona wewe mwislamu unatoa viatu?. Je wewe unamfuata nabii yupi?. Mafundisho ya kutoa viatu umeyapata wapi?

SAHIH MUSLIM VOL 1 HADITHI 1127. UK 277.
Abdullah bin Shakhkhir kuwa alikuwa akiswali na mtume wa Allah, (katika msikitini) kisha akamwona akitema mate na kuyafuta kwa kiatu.

Kunaruhusiwa kusali huku umevaa viatu.
SAHIH MUSLIM VOL 1 HADITHI 1129
Sa’d bin Yazid (Abu Mslama) akimliza mtume Anas bin Malik. Je mtume wa Allah alikuwa akisali na viatu vyake, Anas akajibu Ndio.

7 comments:

  1. we thank Yahweh for the wonderful debate at the famous Tononoka grounds

    ReplyDelete
  2. shukran kwa juhudi zako za kutaka kujua ukweli, walakin mada hii sio ngumu hivyo wala sioni mushkil wowote unaoujadili kwani ingekua bora lau ungesema kuhusu kubudu hali umevua viatu katika imani yenu kwani nyinyi hamuvui kabsaa na imethibiti kua Nabii Issa amani iwe juu yake alikua akivua viatu, walakin unakosa unaposema kua uislam nao umeweka watu wavue viatu wala wasivae viatu, kwani uislam waujua wenyewe wajuzi wa uislam na BORA KAMA HUJUI UISLAM WAULIZE WAISLAM UISLAMU UMERUHUSU KUVAA NA KUTOKUVAA YOTE MAWILI YAMETHIBITI KWA DALILI NAZO NI:- Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam) . SWALAH KWA KUVAA VIATU NA MAAMRISHO YA KUFANYA HIVYO

    "Alikuwa Mtume Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam) akisimama (katika Swalah) bila ya viatu wakati mwingine na kuvaa viatu wakati mwingine"[1]

    Ameruhusu kufanya hivyo kwa Ummah wake na kusema:
    ((Mmoja wenu anaposwali, basi avae viatu vyake au avivue baina ya miguu yake, na wala asimkere mtu kwa viatu hivyo)).[2]

    Aliwasisitizia kuswali na viatu wakati mwingine, na kusema:
    ((Kuweni tofauti na Mayahudi, kwani wao hawaswali na viatu vyao wala na khufu [soksi za ngozi] zao)).[3]

    Mara moja moja alikuwa anavivua wakati anaswali na kisha akiendelea na Swalah yake kama alivyosema Abu Sa'iyd Al-Khudriy:

    "Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) alituswalisha siku moja, na alipokuwa yumo katika Swalah, alivua viatu vyake na akaviweka upande wa kushoto kwake. Watu walipoona hivyo, nao pia wakavua viatu vyao. Alipomaliza kuswali alisema: ((Kwa nini mmevua viatu vyenu?)) Wakajibu: "Tumekuona wewe unavua viatu vyako na sisi pia ndio tukavua viatu vyetu". Akasema:
    ((Hakika Jibriyl alinijia na kunijulisha kwamba kulikuwa na uchafu)) au kasema (kulikuwa na) kitu cha madhara)). Katika riwaya nyingine ((uchafu/ Najsi)) katika viatu vyangu, kwa hiyo nikavivua. Kwa hivyo, mmoja wenu anapokuja msikitini, basi atazame viatu vyake. Akiona vina uchafu, au kasema kitu chenye madhara, na (katika riwaya nyingine) najsi, basi avifute kisha aswali navyo)).[4]

    "Alipokuwa akivivua, alikuwa akiviweka upande wa kushoto kwake.”[5]

    Na pia alikuwa akisema: ((Mmoja wenu anaposwali, asiweke viatu vyake upande wa kulia wala kushoto kwake, ambako vitakuwa katika upande wa kulia wa mwenzake, isipokuwa kama kutakuwa hakuna mtu upande wa kushoto, lakini aviweke baina ya miguu yake)).[6]


    --------------------------------------------------------------------------------




    [1] Abu Daawuud na Ibn Maajah. Ni Hadiyth yenye mapokezi mengi (Mutawaatir) kama alivyotaja atw-Twahaawiy.

    [2] Abu Daawuud na Bazzaar (53, Az-Zawa'id), al-Haakim amekiri kuwa ni Swahiyh na adh-Dhahabiy amekubali.

    [3] Abu Daawuud na Bazzaar.

    [4] Abu Daawuud, Ibn Khuzaymah na al-Haakim ambao wamekiri kuwa ni Swahiyh na adh-Dhahabiy na an-Nawawiy wamekubali. Ya kwanza imetolewa katika Irwaa.

    [5] Abu Daawuud, Ibn Khuzaymah na al-Haakim.

    [6] Abu Daawuud, An-Nasaaiy na Ibn Khuzaymah (1/110/2) na kwa Sanadi iliyo Swahiyh.

    [7] Hii ni Sunnah kuhusu Minbar, kwamba iwe na daraja tatu, na sio zaidi. Kuwa na zaidi ya daraja tatu ni bid'ah iliyoanzishwa na Bani Umayyah. Ni mara nyingi safu hukatika. Na kuliepuka hilo kwa kuiweka pembezoni mwa upande wa Magharibi wa Msikiti au wa Mihraab, ni bid'ah nyingine. Vile vile ni (bid’ah) kuipandisha katika ukuta wa kusini kama roshani ambako mtu hupanda kwa ngazi zilizoshikanishwa na ukuta! Na uongofu mbora kabisa ni uongofu wa Mtumeصلى الله عليه وآله وسلم) ). Tazama Fat-h Al-Baariy (2/331).

    [8] Al-Bukhaariy na Muslim. Riwaya nyingine ni yake Muslim na Ibn Sa'd (1/253). Imetolewa katika “Al-Irwaa” (545).
    arms1423@hotmail.com

    ReplyDelete
  3. marekebisho kwa sentensi ya juu walakin unakosa unaposema kua uislam nao umeweka watu wavae viatu wala wasivue viatu,

    ReplyDelete
  4. english translation the topic praying while wearing shoes or without wearing this normal act in our islamic law and both are allowed , than in your religion only with out foot is being reported :- our evidence on praying while wearing shoes or without wearing shoes:- Prayer Wearing Shoes



    "He Prophet p.b.u.h used to stand (in prayer) bare-footed sometimes and wearing shoes sometimes." [28]



    He allowed this for his ummah, saying:



    «When one of you prays, he should wear his shoes or take them off and put them between his feet, and not harm others with them.»[29]



    He encouraged prayer wearing them sometimes, saying:



    «Be different from the Jews, for they do not pray in their shoes nor in their khuffs (leather socks).»[30]



    Occasionally he would remove them from his feet while in prayer and then continue his prayer, as Abu Sa'eed al-Khudree has said:



    "The Messenger of Allaah (sal-Allaahu 'alayhe wa sallam) prayed with us one day. Whilst he was engaged in the prayer he took off his shoes and placed them on his left. When the people saw this, they took off their shoes. When he finished his prayer he said:



    «Why did you take your shoes off?» They said: 'We saw you taking your shoes off, so we took our shoes off.' He said:



    «Verily Jibreel came to me and informed me that there was dirt - or he said: something harmful - (in another narration: filth) on my shoes, so I took them off. Therefore, when one of you goes to the mosque, he should look at his shoes: if he sees in them dirt - or he said: something harmful - (in another narration: filth) he should wipe them and pray in them.»[31]



    "When he removed them, he would place them on his left" [32] and he would also say:



    «When one of you prays, he should not place his shoes on his right nor on his left, where they will be on someone else's right, except if there is no one on his left, but he should place them between his feet.»[33]





    --------------------------------------------------------------------------------


    [28] Abu Daawood and Ibn Maajah. It is a mutawatir hadeeth as at-Tahaawee has mentioned.



    [29] Abu Daawood and Bazzaar (53, az-Zawaa.id); al-Haakim declared it saheeh and adh-Dhahabee agreed.



    [30] ibid.



    [31] Abu Daawood, Ibn Khuzaymah and al-Haakim, who declared it saheeh and adh-Dhahabee and an-Nawawee agreed. The first one is given in Irwaa' (284)



    [32] ibid.



    [33] Abu Daawood, an-Nasaa.ee and Ibn Khuzaymah (1/110/2) with a saheeh isnaad.

    ReplyDelete
  5. He Jesus peace be upon him told his apostles to go barefoot, without a staff.
    Matthew 10:10
    Provide neither gold, nor silver, nor brass in your purse, Nor scrip for your journey, neither two coats, neither shoes, nor yet staves.

    Luke 9:3
    And he said unto them, Take nothing for your journey, neither staves, nor scrip, neither bread, neither money; neither have two coats apiece

    ReplyDelete
  6. the one who will reply to my comments please let me know so that i will reply back my email is arms142@hotmail.com. thanks i am sure everyone will know the truth and that islam is the true religion.

    ReplyDelete